Friday 22 November 2013

MWONGOZO KWA MH. ZITTO KABWE


CHAMA CHEUPE KUTOKA CONGO CHATOA MWONGOZO KWA ZITTO

Chama Cheupe kinakusihi ujiulize kwamba kilichokuweka kwenye matatizo ni;
 
Mh. Zitto Kabwe.
 1.mambo ambayo yangesababisha kuleta Demokrasia fanisi au demokrasia ya kweli ndani ya Tanzania?

2. ujiulize swali la kwamba unahisi mwanasiasa anastahili kuwa mfano wa Mpelelezi kwa mwingine ndani ya chama?

3. Unahisi watanzania wanatakiwa wamilikiwe na vyama vya siasa ili kuweka taifa katika hali ya kimapambano na mataifa mengine kisera?

4. Unahisi watanzania na viongozi wa vyama vya siasa wanauelewa wa wanachokitaka mwishoni kwa taifa lao na nikwanamna gani watakipima kwamba kimepatikana au kinaelekea kupatikana?

5.Unahisi Revolutions inahusu tuu vyama kwa vyama au hata ndani ya chama na roho za kati ya watu na watu?
 

6. Unahisi watanzania hata viongozi wa vyama vya siasa wanao upeo na uwezo wa kubuni sera zao kama zao bila kukopy kwa mataifa ya nje? na kama hawana ukibuni sera za kwako kama kwako utakuwa matatizoni au hapana?

8.Unahisi mpinzani akijua sera zako za juu ngazi ya chama akazikurupukia kwa kuzitekeleza atafanya vizuri kwa umma au hatafanya vizuri kwa umma?

9.Unahisi kutumiwa ni dhambi au si dhambi? Unahisi una haki ya kutumiwa kwa kuripoti mabaya yenye athari kwa umma tena ambayo hayatakiwi hata kuhasisiwa au si haki ?

10.Unahisi taifa la Tanzania ni kwa sura za leo tuu au hata kwa sura za kesho? kama ni kwa sura za kesho pia utawezaje kulitengeneza bila kuzua zogo ndani ya vyama?

11.je unaamini kuwa anaejaribu kupambana na hesabu hatimae huanguka au unaamini philosophia ya mdomo kupambana na maovu?

12. Unahisi viongozi wengi wa taasisi mbalimbali na watanzania wanadhani tabia za vitu na watu zimesimama au zinazunguruka mfano wa gurudumu? na kama zinazunguruka wamejiandaaje kuendana nazo? kwa sheria? au kwa sera na mipango? na unahisi wao wanadhani kati ya sheria na sera na mipango nini kitaleta ufanisi kwa Taifa.

No comments: