Wednesday 30 October 2013

INAGHARIMU KIASI GANI KUANZISHA BIASHARA?

  • wengi huchagua ujasiliamali?
  • Ni jinsi gani uanzishe biashara ndogo ndogo?

Video hii (Au Bofya Hapa uione kwenye Vimeo) inatueleza si tu mtu asie na kazi ndie awe mjasiliamali bali hata walioko maofisini wanajishughulisha. Utasikia ushauri pia kwa wanawake kutoka kwa Madam Shammy.


Watu wengi katika ulimwengu wa sasa,wawe waajiriwa ama lah! wamegundua ujasiliamali  ndio "BIG DEAL".Utajiuliza kwanini?

  1. Faida: Baina ya wajasiliamali waliopata na wanaoendelea kupata faida kubwa nchini Marekani ni pamoja na Bill Gate, mmiliki wa Microsoft Corporation na Sam Walton mmiliki na mwanzilishi wa Wal-malt. Unawezakuwa miongoni mwa watanzania wengi ambao pia hupata faida kubwa kila mwaka kwa shughuli za ujasiliamali.
  2. Fursa: Hii ni moja ya sababu kubwa inayohamasisha watu kuacha kazi na kujiajiri wenyewe. Fursa zipo ktk nyanja mbalimbali iwe kilimo, elimu, biashara, ujenzi n.k je, wewe ndoto yako ni kuwekeza au kuwa na biashara yako?acha kuota, amka!!
  3. Changamoto: Asilimia kubwa ya wajasiliamali hutafuta zaidi mafanikio kuliko uongozi au umaridadi. Ujasiliamali sio kamali, hasara ni moto na sehemu ya kukomaa (kukua) zaidi kama si kujifunza.
  4. Uhuru: Watu wengi hawanauhuru na furaha kufanya kazi katika kampuni au watu binafsi na hata serikalini kwa kuepuka presha na "stress" huanzisha na huridhika na shughuli zao binafsi.
  5. Ukosefu wa ajira: Vijana wengi wa kitanzania wameamka na hata kugeukia upande wa pili wa shilingi baada ya ukosefu wa ajira na kujikuta wakiendelea kuzunguka na bahasha zao bila mafanikio.
  6. Vipaji (Talent): Wapo walogundua kuwa kwa kuajiriwa wanakosa fursa ya kutumia vipaji vyao ambavyo vingiweza kuwalipa zaidi.
Fuatilia picha hizi zinazomhusu Kijana Zawadi na mwenzake walivyoweza kujiajiri hapa Jijini Mbeya 
                                                                                                                                    
Juu: Huyu ndiye Zawadi kijana alietokea kutembeza katika begi la mgongoni culture (cheni zilizotengenezwa kwa shanga na nyuzi, kofia) hadi kufungua ofisi yenye kutembelewa na idadi kubwa ya watalii, Arts and Tribues Tours.


Juu: seti ya kochi imetengenezwa kwa kamba za porini.


Juu: Stendi na vikapu vya maua vinavyotengenezwa kwa malighafi zipatikanazo hapa hapa nchini.



Kushoto: 'coffee table' inayotengenezwa pia kwa mianzi, miti na kamba za porini na kuuzwa kwa bei nafuu sana. 














Kulia: Ni vitambaa, posti kadi na picha zilizochorwa kwa mikono.



Kushoto: Viti vya asili vilivyochongwa kwa mninga.














  Jinsi ya kuanzisha biashara 

Biashara nyingi ndogo ndogo huanzia nyumbani lakini ili uwe na biashara yenye mafanikio zingatia yafuatayo;
  • Weka wazo la biashara unayotaka kufanya katika maandishi na mpangilio mzima wa jinsi unavyotaka biashara yako iwe.
  • Andaa mchanganuo wa biashara (business plan).
  • Uwe na mtaji haijalishi mkubwa au mdogo pamoja na rasilimali watu (employee or partners).
  • Tambua wateja wako, hali ya soko na sehemu soko lilipo.
  • Weka rekodi ya mahesabu ya shughuli zako (accounting). Hii itakusaidia kutambua kama unafanya biashara kwa kukua au hasara.  

Monday 28 October 2013

TREES, OUR LIVES AND OUR BEST FRIEND

  • Tree Farming
  • Where do oldest and largest things found in the world?
  • What are the importance of trees?
Tree is the largest of all plants which continue to grow as long as they live.
 People do not think of trees the way they think of other plants most of which grow only a short time and then die. They think of trees as permanent parts of the landscape. Year after year trees provide shades to houses and streets from the sun hence we should change and have positive attitudes and plans towards trees for our generations.

                                           
USES OF TREES

 Wood products :  Each year loggers cut down millions of trees from different forests to Sawmills. Sawmills cut these logs into lumbers, which manufactures use for construction works, paper making, furniture, alcohol and plastics are as well products from trees.

Food Production : People throughout the world eat fruits such as avocados, oranges, mangoes, grapes, apples, cherries and peaches. Also nut tree (coconut palm) produces coconuts. Trees`also supply chocolate, coffee, maple syrup, olives, spices such as cinnamon and cloves.

Other tree products : The tree produces Latex, a milky fluid used to make natural rubber. Pine trees produce sticky resin used in making turpentine. The bark of oak and some other trees contains a compound called tannic acid which is used by tanning industries to change animal hides into lather. Some tree products are used as medicines for instance the bark of the cinchona tree contains quinine which doctors use to treat malaria and other diseases.

Who denies?
The World is the best place to live especially when trees are all over around us.

Trees in conservation : Trees help to conserve soil and water, in open country trees act as windbreaks and keep the wind from blowing the topsoil. Tree roots store water in the ground but also prevent soil from being washed away. In mountain regions, forests prevent erosion and provide shelter for wildlife and recreation areas for vacationists.
The most important role of trees is balancing of gases (Oxygen and Carbondioxide) in the atmosphere which is the necessary process for our lives.

 TREE FARMING

A tree farm is a privately owned area used to grow forest crops for profit. The owner must show that the timber will be grown and harvested in such a way that crops can also be grown on the land in the future, protect from diseases, fire, excessive grazing and other damage.

Note: Among the oldest and largest trees of thousands of years and over 200feet (61meters) tall are in California.
  

Wednesday 23 October 2013

START AND BE YOU


STOP THINKING, START ACTING!
  •  Is not a challenge but an opportunity.
Being someone else is absolutely insane.You should of course live your dreams and be yourself. 
You have plans and ideas in your head and perhaps you have dreams to accomplish, yet you are scared of turning them into reality, "youth unemployment" is your morning prayer; guess what? You will die with them all. Real minds dare to try and failing is just a challenge which make them stronger and eager to fulfill whatsoever started. Being ready to take risks of your new investment is the best character. Every employer is a capitalist, don't turn to be his/her slave. Explore your mind, with full energy make your ideas work. With time you will be another person.

There are people who will discourage you, laugh at you and wrongly advice you, you shouldn't drop to their level as you were not made to live up their thoughts nor their expectations. Stand up tall for whatever idea you wish to work on. Change your ways of thinking and attitude to attain goals of your project / idea. With all what you have you can, you should constantly ponder the goals you truly need to accomplish.

THAT'S HOW IT TAKES TO BE AN ENTREPRENEUR!

 
"The secret of change is to focus all of your energy, not on fighting the old but on building the new" Socrates

Monday 21 October 2013

JE WAJUA?

DARAJA LA MUNGU, MBALIZI
  • Limeundwa kwa mawe.
  • Ni imara na linamiaka mingi zaidi
  • Halijawahi athiriwa na tetemeko la ardhi au mmomonyoko wa udongo
Daraja la Mungu liko Mbeya, Mbalizi katika kijiji cha Sisitila. Chakushangaza wenyeji wengi hawatambui kama ni kivutio kikubwa kwa wageni (watalii) kutokana na maajabu ya daraja hili.



Chini ya daraja hili kuna mto ambao umekua na manufaa makubwa kwa wakazi wa kijiji cha Sisitila na Wimba kwani wameweza kufanya kilimo cha umwagiliaji wa mbogamboga na vitalu vya miti pamoja kunyweshea mifugo. Kama inavyoonesha katika picha upande wa kulia ni mfereji ambao unatumika kuchukua maji kutoka katika mto na kupeleka shambani.      Picha kushoto: Shamba la mbogamboga.














Kwa wakazi wa mkoa wa Mbeya, kama mtakumbuka Disemba, 1997 wakati wa mvua kubwa za El Nino daraja la mto Mbalizi katika eneo la Mbalizi , Mbeya lilibomoka kwa mafuriko mbali ya kuwa na mifereji mitatu lakini DARAJA LA MUNGU halikutetereshwa na mvua wala mafuriko hayo............AJABU!!!!!

 Yawezekana mizizi ya mti huu ni moja ya vizuizi vya mmomonyoko wa udongo katika daraja hilo.
Baadhi ya mifugo ikiswagwa kuelekea katika mto unaopita chini ya daraja la Mungu.
Baadhi ya mawe yaliyochanganyika na udongo na kuunda daraja hilo.

Sunday 20 October 2013

ORODHA YA SHULE ZA SEKONDARI WILAYA YA MBOZI, MBEYA,.

ORODHA YA SHULE ZA SERIKALI 

1.     BARA                         0754369361
2.     CHIKANAMLILO           0788546190
3.     CHITETE                    0764948802
4.     HALUNG                     0766010141
5.     IDIMI                         0755063284
6.     IGAMBA                     0766862734
7.     IGANYA                      0766482006
8.     IGANDUKA                 0784267769
9.     IHANDA                     0762936606
10. ILOLO                        0754871438
11. IPUNGA                     0787847519
12. ISANGU                     0756582044
13. ISANDULA                  0755077347
14. ITAKA                        0765304928
15. ITUMPI                      0754464624
16. IVUNA                       0766895504
17. J.M KIKWETE              0754514009
18. KAPELE                      0754049051
19. LWATI                       0756512575
20. J.K NYERERE               0754917665
21. MLANGALI                  0755709474
22. MLOWO                     0754080323
23. MPAKANI                   0755535637
24. MPEMBA                    0757579877
25. MKULWE                    0755386844     
26. MSANGANO                 0755987221
27. MSANGAWALE             0784216609
28. MSANKWI                   0757304465
29. MSENSE                     0765061290
30. MSIA                         0786174349
31. MYOVIZI                    0755961156
32. MOMBA                      0755649795
33. NAMBINZO                 0754091474
34. NANSWILU                 0753122567
35. NALYELYE                  0784658470
36. NDUGU                      0755656150
37. NYIMBILI                   0754636708
38. SHAJI                        0758039085
39. SHIWINGA                 0789627575
40. SIMBEGA                   0763445505
41. UWANDA                    0784342394
42. VWAWA                     0784997038
43. INSANI                      0784541321
44. ISALALO                    0758253393
45. NZOVU                      0756054136
46. HEZYA                       0766866567
47. HAMPANGALA             0755203344
48. ITEPULA                     0754595856
49. KILIMAMPIMBI            0754527830
50. LUMBILA                    0784527512
51. SHIKULA                    0784522689
52. NKANGA                     0755049980
53. NKANGAMO                 0754212495
54. NAMOLE                     0753700140

ORODHA YA SHULE BINAFSI

1.     CANAAN                     0754584145
2.     HASANGA                   0754806409
3.     HOLLYWOOD              0755510202
4.     IDIGIMA                    0757182437
5.     ILASI                         0762446694
6.     ISANSA                      0755179844
7.     IYULA                        0754144714
8.     JAMES SANGU             0754695903
9.     MAHENJE                   0752800253
10. MBOZI                      0756652710
11. NDYUDA                    0754552967
12. NG'AMBA                   0754452886
13. OSWE GIRLS'             0752398224
14. THOMAS MORE           0754912200
15. TUNDUMA                  0754912237
16. WIZA                        0758047720


Friday 18 October 2013

TWEET OF THE DAY!!!!

Trees around us give fresh air, cool wind and shades during day time. Rain formation also includes trees which in turn water our fields. Despite the full understanding on the importance of trees:

Wednesday 2 October 2013

UKISTAAJABU YA MUSA..............

UKISTAAJABU YA MUSA...............


  • NI NYANI JAMII YA NGEDERE AISHIE KATIKA FAMILIA MOJA NA BINADAMU
  • NI WATANZANIA WACHACHE WENYE "HOBBY" NA UPENDO KWA WANYAMA
  • HUENDA SALUNI,HULA PAMOJA NA BINADAMU NA PIA HUPATIWA MATIBABU KAMA BINADAMU.
  • ANAITWA JACKSON "JACKY" 
 JL Company ilivutiwa na maisha ya Jacky na imedhamiria kumsaidia katika chakula na dawa ila pia mashuka ya kulalia na godoro. 

Endelea Kusoma na Ushuhudie Maajabu ya Jacky katika.................


Happy ndie mlezi mkuu wa Jacky. wakiwa njiani kuelekea saluni pamoja kwa. Jacky ana umri wa mwaka mmoja sasa. 
Jacky akiandaliwa kwa ajili ya kuogeshwa. Ngedere huyu anatabia kama mtoto mdogo, huchagua mtu anaemfahamu amuogeshe na huwa mkali sana na hata kugoma kuoga endapo ataogeshwa na mtu asiemfahamu. ni mcheshi sana na hupenda kucheza na kila mtu.
Jacky baada ya kuoga akiwa na mlezi wake.
Kadanganyishiwa mkate ili apakwe mafuta na kuchanwa nywele (manyoya.)
Mtoto akilia mama hulazimika kumnyonyesha au kumpa uji. Jacky pia alilia njaa wakiwa wanaendelea na shughuli za saluni hivyo alipewa chakula kama aonekanavyo katika picha.ameketi kwa nidhamu na utulivu akila   ( table manners applied)
Jacky ni rafiki wa watoto na mara nyingine si kucheza pamoja tu bali hula pamoja.


"Jacky ni sehemu ya familia yangu, tunakula pamoja na kucheza pamoja. Ni msafi sana kila asubuhi anapiga mswaki na anajua wapi ajisaidie haja ndogo na kubwa. Itokeapo kaumwa ni rahisi kumgundua kwani huwa mtulivu na hupunguza kula au hugoma kabisa kula. Na ameshawahi umia pia, alipigwa na gongo na mtoto wa jirani kitu kilichopelekea kuvuja damu nyingi puani na kuvimba mguu. Nilimchua mguu na kumpa dawa ya maumivu ( diclofenac) lakini alimchukia sana yule mtoto na hata alipojaribu siku nyingine kucheza nae Jacky alimng'ata kwa kujihami." alisema Happy.
Haya ni maajabu kwa watanzania wengi. Je, wewe ungeweza?